Wapendwa leo tutaangalia kidogo upande tofauti, naule tuliozoea, leo tuko upande wa mazingira, kwani endapo tutayaboresha basi na shughuli zetu za kiujasiriamali zitaweza kufanyika vizuri sana, karibu sasa twende pamoja.






Mazingira ni mambo yote yanayo athiri ukuaji au uwepo wa viumbe hai,mfano hewa,maji na ardhi.Mazingira ni kitu muhimu sana katika ustawi wa viumbe hai wowote,katika dunia hii tuliyomo.Mazingira ni muhimu kwa ukuwaji ya mimea mbalimbali,viumbe wabaharini,viumbe walioko chiniya ardhi,na viumbe walioko juu ya uso wa dunia.

Sera mbalimbali za uifadhi wamazingira na viumbe vyake zimewekwa kwa lengo mmoja kubwa kwanza kutunza mazingira lakini pili kulinda aina ya viumbe waliomo(species).Mfano sera ya mazingira ya mwaka 1997 ina tamka wazi na inazitaka wizara zote namtu mmoja mmoja kuweka au kuchanganya swala la mazingira katika miradi yao au katika shughuli zao,yani lazima kuwe na  ‘equal balance’maendeleo katika shughuli zao  lakini na hakikisho la kuweka mazingira endelevu kwa ajili ya maisha yaviumbe hai.




Sera yaelimu na mafunzo ya mwaka 1996, inazitaka taasisi zote za elimu kuongeza uelewa wa maswala yamazingira kwalengo la kuendelezaupatikanaji wa taarifa linapokuja suala la kufanya maamuzi kwenye jambo la mazingira.

Pia kwenye suala la kulinda viumbe hai mfano nyuki, sera inasema hivi, “any investment that takes place inside or around bee reserves and apiaries don’t pose potential damage or danger to bees,bee products and bee fodder plants”.Tafsiri isiyo rasmi ni kwamba, uwekezaji wowote unao fanyika ndani au eneo la hifadhi ya nyuki na kwenyemizinga yao, usiharibu au kuhatarisha nyuki pamoja na malisho yao.


Kwa hiyo kwa na mnamoja au nyingine tuna ona umuhimu wa kutunza mazingira kwa faida yetu na viumbe hai vinavyo tuzunguka kwakuwa sisi soteni mazingira na mazingira ni sisi.


Faida ya moja kwa moja tunayo pata kwa kutunza mazingira vizuri ni kuongeza umri wa kuishi katika ulimwengu huu tulionao na kuishi kwa raha mstarehe.

Maisha yetu yamekuwa mafupi kwa sababu tumearibu mazingira. Kunauhusiano mkubwa kati ya umri wa maisha yetu na  uhifadhi wa mazingira,maisha yetu yanakuwa mafupi kwa sababu tuna kula vitu visivyo na ubora na ambavyo avijengi mwili bali kuharibu mwili, na vyakula hivyo havina ubora kwa kuwa ardhi inayotoa hayo mazao imeharibiwa na shughuli za binadamu. Kwa hiyo ardhi haina rutuba, yaasili, ina bidi tuweke mbolea za viwandani ili angalau kuifanya au kuirudishia tena rutuba kama ile ya mwanzo, ili ituletee mazao bora kwa ajili ya afya zetu, kitu ambacho ni kigumu sana, kurudisha ualisia wa awali.


Jambo linguine kubwa tunalo nufaika nalo endapo  tutajitaidi kutunza mazingira, ni hakikisho la viumbe hai vyote kwa maana mazao yamisitu na wanyama ambayo kwayo, uwepo wake una tufanya tutegemeane wote, yani miti na viumbe wengine wanatutegemea binadamu katika kuendelea kuwepo, na sisi tuna vitegemea viumbe hivi ili tuendelee kuwepo.


Kwa hiyo ni muhimu kujitaiditi kutunza mazingira kwa faida yangu nayako.


Nini cha kufanya kwa wale ambao ili maisha yao yaende kilasiku inabidi  waaribu mazingira? Kuna njia angalau za kufanya ili kupunguza uharibifu wa mazingira, mmoja wapo ni kufanya/kugeuza au kudurufu takataka na kuwa malighafi tena kwa ajili ya kutumia(recycle), mfano karatasi zisizotumika zinaweza kulowekwa kwenye maji alafu zikikaushwa zina weza kutumika kama mkaa, maji machafu yanaweza kugeuzwa kuwa maji safi tena, ingawa ukweli baadhi yahizi njia zinaitaji utaalamu kidogo, lakini kama una nia utafanikiwa, jaribu kuwaona watukama SIDO,TATEDO,wanaweza kukupa msaadazaidi nini cha kufanya ili kufikia kufanya mapinduzi ya kijani.


Maranda ya mbao yana wezakugeuzwa na kuwa bidhaa bora ya kupikia ikawa badalaya kukata kata kuni ovyo. Mbolea ya wanyama kama ngo’mbe ukipata utaalamu kidogo kwa watu nilio kwa mbia ina weza kukusaidia kupata nishati nzuriya kupikia ikawa ni mmbadalawa kuni, hata uchafu wa jikoni  kama maganda ya vitunguu, nyanya mabaki ya vyakula kwa namna moja au njingine vina weza kubadilishwana kuwa nishati, kuna watu wanautaalamu wa kufanya shughuli hizi kwa mfano Dr.Didas wa MJASIRIAMALI KWANZA, wanaweza kukupa utaalamu huu, na wewe ukaishi kwa raha mstarehe.